» » KINGA DHIDI YA SARATANI



KINGA DHIDI YA SARATANI
Nkukurah, D. K
nkukurahd@yahoo.com , nkukurah blogspot.com

Tafsiri ya neno saratani
Saratani ni mgawanyiko  mbaya wa uzalishaji na usambaaji wa chembe chembe hai zisizo za kawaida ndani ya mwli.

Aina kuu za saratani:
Saratani ya mapafu
Saratani ya ngozi
Saratani ya shingo ya uzazi kwa wanawake
Saratani ya matiti kwa wanawake
Saratani ya tezi dume
Saratani ya matumbo
Saratani ya midomo kwa wavuta sigara
Viashilia hatarishi:
C – Mabadiliko katika upatikanaji wa haja kubwa
A – Vidonda visivyopona
U –Kutokwa na damu/majimaji/usaha usiokuwa wa kawaida
T –Uvimbe kuwa mgumu au kuongezeka kwa ukubwa
I –Shida ya kusaga chakula tumboni au kumeza
O –Mabadiliko ya wazi kwa uvimbe uliokuwa nao siku nyingi
N –Kikohozi kisumbufu au sauti kukwaruza

Visababishi Vikuu:
1. Mionzi
2. Kemikali
3. Baadhi ya Bakteria na Virusi
4. Chakula (Fangasi na Additives)
5. Tumbaku na sigara
6. Pombe
Visababishi hivi vikuu husababisha uokisidishaji wa molekuli za mwili na kuzifanya kuwa radikali huru. Radikali huru uanzisha mapambano dhidi ya molekuli zingine na kuzifanya kuwa radikali huru pia. Mchakato huu ukiendelea bila kudhibitiwa mapema utengeneza radikali huru nyingi mwilini ambacho hugeuka kuwa chembechembe za saratani. Angalia mchoro huu hapa chini.





Kudhibiti mchakato wa uokisidishaji
Ili kudhibiti mchakato wa uokisidishaji ni kukubali kula vyakula vyenye vipinga uokisidishaji. Vyakula hivi ni vyepesi na rahisi, pia vinapatikana katika mazingira yetu ya kawaida kwa bei nafuu. Kwa kufanya hivyo utakuwa umejiweka katika mazingira mazuri ya kujikinga dhidi ya saratani.rejea jaribio dogo lililofanywa kuthibitisha uokisidishaji kwenye tunda la epo lililopasuliwa katikati, upande mmoja kupakwa maji ya limao yenye wingi wa vitamin C na upande mwingine kuachwa wazi na kuruhusu uokisidishaji kutokea. 



Ifuatayo chini ni orodha ya vipinga uokisidishaji:-
1. vitamin
Vitamin  A: Vyanzo vikuu; Karoti, skwashi, brokoli, viazi vitamu, nyanya,  boga, pichi na aprikoti
Vitamin  C: Vyanzo vikuu;  machungwa, limao, chenza, embe , nanasi, ndizi, epo, pilipili za kijani, brokoli, mboga za kijani, strobeli  na nyanya,.
 Vitamin E: Vyanzo vikuu; mbegu (Nuts and seeds), nafaka, mboga za kijani

2. Madini  ya Selenium
Vyanzo vikuu; samaki, mtama,mayai, na vitunguu shwaumu

3. Kemikali za mimea
Kemikali ya Flavenoids . Vyanzo vikuu; Maharage, zabibu za zambarau, komamanga,kreni beli, chai
Kemikali ya Lycopene. Vyanzo vikuu; Nyanya, barungi za pinki, na tikiti maji
Kemikali ya Lutein. Vyanzo vikuu; mboga za majani mfanoo; brokoli, na spinachi


Share/Bookmark

Kuhusu Unknown

Habari!Karibu upate maarifa zaidi .
«
Next
This is the most recent post.
»
Previous
Older Post

No comments:

Andika maoni